• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Pigo kwa Barcelona fowadi Braithwaite akiungana na Aguero na Fati mkekani kuuguza majeraha

Pigo kwa Barcelona fowadi Braithwaite akiungana na Aguero na Fati mkekani kuuguza majeraha

Na MASHIRIKA

FOWADI Martin Braithwaite wa Barcelona atafanyiwa upasuaji wa goti katika hatua ambayo ni pigo kubwa kwa waajiri wake msimu huu ikizingatiwa kwamba Sergio Aguero pia anauguza jeraha la goti.

Nyota huyo raia wa Denmark mwenye umri wa miaka 30 aliumia goti la kushoto katika ushindi wa 2-1 uliosajiliwa na Barcelona dhidi ya Getafe katika mchuano wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Agosti 29, 2021.

Kwa mujibu wa Barcelona wanaotiwa makali na kocha Ronald Koeman, hatua ya Braithwaite kufanyiwa upasuaji inachukuliwa baada ya tiba ya kawaida kushindikana.

Aguero, 33, anatarajiwa kuwa nje hadi Oktoba 2021.Fowadi chipukizi raia wa Uhispania, Ansu Fati, 18, pia hajawajibikia Barcelona katika mchuano wowote msimu huu kwa kuwa anauguza jeraha la goti.

Kutokuwepo kwa Aguero na Fati kulifanya Braithwaite na Memphis Depay kuwa washambuliaji tegemeo wa Barcelona katika mechi tatu zilizopita za La Liga. Braithwaite ambaye ni mchezaji wa zamani wa Middlesbrough alifunga mabao mawili katika mchuano wa ufunguzi wa msimu huu dhidi ya Real Sociedad.

Barcelona wamepangiwa kuvaana na Bayern Munich katika mechi ya makundi ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Septemba 14, 2021 uwanjani Camp Nou, Uhispania.

  • Tags

You can share this post!

Demba Ba aangika daluga zake katika ulingo wa soka

UEFA: Vipusa wa Chelsea na Arsenal wafahamu wapinzani wao...