• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 11:50 AM
UEFA: Vipusa wa Chelsea na Arsenal wafahamu wapinzani wao msimu huu

UEFA: Vipusa wa Chelsea na Arsenal wafahamu wapinzani wao msimu huu

Na MASHIRIKA

CHELSEA waliokuwa wanafainali wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwa wanawake mnamo 2020-21 wametiwa katika Kundi A pamoja na Wolfsburg, Juventus na Servette muhula huu.

Arsenal kwa upande wao wametiwa katika zizi moja na Barcelona waliowapepeta Chelsea kwenye fainali ya msimu uliopita. Miamba hao watavaana pia na Hoffenheim pamoja na Koge.

Chelsea waliwapiga Wolfsburg ambao wamenogesha fainali za kipute hicho mara tano tangu 2013 kwenye robo-fainali za UEFA mnamo 2013, hiyo ikiwa mara yao ya nne kukutana chini ya kipindi cha misimu sita.

Hii ni mara ya kwanza kwa mapambano ya UEFA miongoni mwa wanawake kuanza kwa hatua ya makundi. Kampeni za kuwania ubingwa wa taji hilo zimeratibiwa kuanza kati ya Oktoba 5-6 na kukamilika Disemba 15-16, 2021.

Vikosi viwili vya kwanza vitasonga mbele na kuingia hatua ya robo-fainali.Chelsea walifuzu kwa kampeni za muhula huu baada ya kuibuka mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (WSL) huku Arsenal waliokuwa mabingwa wa UEFA mnamo 2007 wakiambulia nafasi ya pili.

Lyon waliokuwa mabingwa wa UEFA mara tano mfululizo hadi kufikia mwanzo wa msimu wa 2020-21 wametiwa katika Kundi D kwa pamoja na Bayern Munich.

Real Madrid watakwaruzana na Paris St-Germain, Breidablik na Kharkiv katika Kundi B.

DROO YA UEFA 2021-22:

KUNDI A: Chelsea, Wolfsburg, Juventus, Servette

KUNDI B: Paris St-Germain, Breidablik, Real Madrid, Kharkiv

KUNDI C: Barcelona, Arsenal, Hoffenheim, Koge

KUNDI D: Bayern Munich, Lyon, Hacken, Benfica

  • Tags

You can share this post!

Pigo kwa Barcelona fowadi Braithwaite akiungana na Aguero...

Congo yajifua kubaki ligini, Buruburu ikilia maamuzi ya...