Na MASHIRIKA
LIONEL Messi, Neymar Jr na Kylian Mbappe walifunga mabao na kusaidia waajiri wao Paris St-Germain (PSG) kupepeta Maccabi Haifa ya Israel 3-1 katika pambano la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Jumatano usiku.
Tjaronn Chery aliwaweka Maccabi uongozini katika dakika ya 24 kabla ya Messi kusawazisha mambo kunako dakika ya 37.
Mbappe alicheka na nyavu za wenyeji wao katika dakika ya 69 kabla ya Neymar kuhakikisha kwamba wanaondoka Israel na alama tatu muhimu ambazo sasa zinawadumisha kileleni mwa Kundi H kwa alama sita, saw ana Benfica ya Ureno waliokomoa Juventus 2-1 nchini Italia.
Messi kwa sasa amefunga bao dhidi ya vikosi 39 tofauti katika soka ya UEFA. Mtani wake mkuu, Cristiano Ronaldo, amefunga dhidi ya timu 38 tofauti na ndiye sogora wa kwanza kuwahi kufunga bao kwenye UEFA katika misimu 18 tofauti.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO