• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 9:50 AM
PSG yakomoa Nantes na kujizolea taji la Trophee des Champions nchini Ufaransa

PSG yakomoa Nantes na kujizolea taji la Trophee des Champions nchini Ufaransa

Na MASHIRIKA

NYOTA Neymar alifunga mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kunyanyua taji la Trophee des Champions baada ya kucharaza Nantes 4-0 mnamo Jumapili usiku jijini Tel Aviv, Israel.

Pambano hilo lilikuwa la kwanza kwa kocha Christophe Galtier kusimamia kambini mwa PSG tangu aaminiwe kuwa mrithi wa Mauricio Pochettino aliyepigwa kalamu mwanzoni mwa Julai.

Mabao mengine ya PSG yalijazwa kimiani kupitia kwa beki Sergio Ramos na Lionel Messi aliyeshirikiana vilivyo na Neymar.

PSG ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1), sasa wameshinda mataji tisa kati ya 10 yaliyopita ya Trophees des Champions. Kipute hicho ni cha hadhi sawa na gozi la Community Shield ambalo huashiria mwanzo wa msimu mpya katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). Nantes walifuzu kwa kivumbi cha Trophees des Champions muhula huu baada ya kuzoa taji la French Cup msimu wa 2021-22.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Mwendeshaji bodaboda afariki katika ajali Kirinyaga

BENSON MATHEKA: Uchaguzi mkuu sio mzaha, tujitokeze kwa...

T L