• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
Rangers wadengua RB Leipzig na kufuzu kwa fainali ya Europa League

Rangers wadengua RB Leipzig na kufuzu kwa fainali ya Europa League

Na MASHIRIKA

RANGERS watavaana na Eintracht Frankfurt kwenye fainali ya Europa League msimu huu.

Hii ni baada ya kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Scotland kupokeza RB Leipzig kichapo cha 3-1 mnamo Alhamisi usiku jijini Ibrox na kudengua miamba hao wa Ujerumani kwa jumla ya mabao 3-2 kwenye nusu-fainali.

Baada ya kupepetwa 1-0 katika mkondo wa kwanza, Rangers walichuma nafuu katika uwanja wao wa nyumbani na wakaiiweka kifua mbele katika dakika ya 18 kupitia kwa James Tavernier. Glen Kamara aliwafungia bao la pili kunako dakika ya 24 kabla ya Leipzig kurejea mchezoni kupitia kwa Christopher Nkunku aliyepachika wavuni goli lake la 32 msimu huu. John Lundstram alifunga bao la tatu la Rangers katika dakika ya 80.

Chini ya kocha Giovanni van Bronckhorst, Rangers sasa watakutana na Frankfurt katika fainali itakayochezewa jijini Seville, Uhispania mnamo Mei 18, 2022.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

KASHESHE: Ezekiel Mutua arudisha ngori

LEONARD ONYANGO: Pana hatari ya baa la njaa kuzidi...

T L