• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:55 AM
Rangers yalenga rekodi ya kukamilisha msimu bila kulimwa

Rangers yalenga rekodi ya kukamilisha msimu bila kulimwa

Na MASHIRIKA

KOCHA Steven Gerrard amewataka wanasoka wake wa Rangers kuweka historia kwa kukamilisha kampeni za Ligi Kuu ya Scotland msimu huu bila ya kushindwa.

Mabingwa hao wa Scotland wanatarajiwa kualika Aberdeen katika mechi ya mwisho ya muhula huu mnamo Mei 15 baada ya kuwapepeta Livingston 3-0 mnamo Jumatano usiku.

Penalti ya James Tavernier na mabao mengine kutoka kwa Ryan Kent na Ianis Hagi yaliwezesha Rangers kupiga mchuano wao wa 25 ligini bila ya kufungwa bao huku wakifikisha jumla ya alama 99.

“Rangers hawajawahi kujizolea zaidi ya alama 100 kwenye Ligi Kuu ys Scotland. Kiu ya kuweka rekodi hiyo, baada ya kuweka rekodi nyingine ya mechi nyingi zaidi bila ya kufungwa, inatarajiwa kutupa msukumo na motisha zaidi katika gozi la mwisho dhidi ya Livingston,” akasema Gerrard ambaye ni kiungo na nahodha wa zamani wa Liverpool.

Rangers watapokezwa taji la Ligi Kuu ya Scotland mwishoni mwa mechi ijayo dhidi ya Aberdeen na Gerrard amewataka mashabiki wa kikosi chake kutovuruga sherehe ya kutawazwa kwao kwa kutofika ugani.

Livingston wangali na matumaini ya kuwaruka St Johnstone na kukamilisha kampeni za ligi msimu huu katika nafasi ya tano. Vikosi hivyo vitapimana ubabe katika mechi ya mwisho msimu huu wa 2020-21 mnamo Mei 15.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Commander Okoth atinga nusu-fainali ya ndondi za Urusi

Nahodha wa zamani wa Man-United, Antonio Valencia, astaafu...