• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 5:04 PM
Real Madrid wapepeta RB Leipzig ya Ujerumani katika gozi la UEFA

Real Madrid wapepeta RB Leipzig ya Ujerumani katika gozi la UEFA

Na MASHIRIKA

REAL Madrid walihitaji mabao mawili ya dakika za mwisho ili kukomoa RB Leipzig ya Ujerumani 2-0 katika gozi la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).

Ushindi huo ulimfanya Carlo Ancelotti kuwa kocha wa pili kushinda mechi 100 za UEFA.

Leipzig walipoteza nafasi nyingi za wazi huku fowadi wao tegemeo Christopher Nkunku akizidiwa ujanja na kipa Thibaut Courtois mara mbili.

Federico Valverde aliwaweka Real kifua mbele katika dakika ya 80 baada ya kukamilisha krosi safi aliyomegewa na Vinicius Jr.

Marco Asensio alipachika wavuni bao la pili la Real kutokana na krosi ya Toni Kroos.

Hii ni mara ya kwanza tangu 2017-18 kwa Real kushinda mechi mbili mfululizo za ufunguzi katika UEFA.

Ni mkufunzi Alex Ferguson aliyewahi kunoa Manchester United ambaye anajivunia rekodi ya kushinda mechi nyingi zaidi za UEFA (102).

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Aliyefukuza babake ashtakiwa

Haaland atambisha Man-City dhidi ya Borussia Dortmund...

T L