• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Ronaldo aweka rekodi ya ufungaji wa mabao Ulaya

Ronaldo aweka rekodi ya ufungaji wa mabao Ulaya

Na MASHIRIKA

NYOTA Cristiano Ronaldo alifunga bao lake la 20 katika kampeni za Ligi Kuu ya Italia (Serie A) mnamo Jumanne usiku na kusaidia waajiri wake Juventus kusajili ushindi wa 3-0 dhidi ya Spezia jijini Turin.

Mechi hiyo ilikuwa ya 600 kwa Ronaldo kusakata katika taaluma ya usogora kwenye ngazi ya klabu.

Mabao yote matatu ya Juventus ya kocha Andrea Pirlo yalifumwa wavuni katika kipindi cha pili. Alvaro Morata alifungulia mabingwa hao watetezi wa Serie A ukurasa wa mabao katika dakika ya 62 baada ya kukamilisha krosi ya Federico Bernardeschi.

Federico Chiesa alifunga bao la pili kunako dakika ya 71 kabla ya Ronaldo kuzamisha kabisa chombo cha wageni wao mwishoni mwa kipindi cha pili.

Ushindi kwa Juventus uliwapaisha hadi nafasi ya tatu kwa alama 49, saba nyuma ya viongozi Inter Milan inayonolewa na kocha wa zamani wa Chelsea, Antonio Conte.

Ni pengo la pointi tatu kwa sasa ndilo linatamalaki kati ya Juventus na nambari mbili AC Milan.

Bao lililofungwa na Ronaldo dhidi ya Spezia sasa linamfanya kuwa mchezaji wa kwanza kuwahi kufikisha idadi ya mabao 20 katika kila mojawapo ya misimu 12 iliyopita kwenye Ligi Kuu tano za soka ya bara Ulaya.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Dortmund wapiga Gladbach na kutinga nusu-fainali za German...

Marseille wamfuta kazi kocha Villas-Boas na kumwajiri Jorge...