• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 5:15 PM
Dortmund wapiga Gladbach na kutinga nusu-fainali za German Cup

Dortmund wapiga Gladbach na kutinga nusu-fainali za German Cup

Na MASHIRIKA

CHIPUKIZI Jadon Sancho alifunga bao la pekee na la ushindi katika mechi iliyowawezesha waajiri wake Borussia Dortmund kuwabandua Borussia Monchengladbach kwenye robo-fainali za German Cup mnamo Jumanne usiku.

Sancho ambaye ni fowadi wa Uingereza alicheka na nyavu za wenyeji wao katika dakika ya 66. Bao la fowadi Erling Braut Haaland lilifutiliwa mbali na refa katika dakika ya 34 baada ya teknolojia ya VAR kubaini kwamba alicheka na nyavu akiwa ameotea.

Wenyeji pia walishuhudia bao walilofungiwa na Marcus Thuram likifutiliwa mbali na VAR.

Kichapo ambacho Gladbach walipokezwa kilikuwa chao cha nne mfululizo tangu mkufunzi wao Marco Rose kutangaza kwamba atakuwa akijiunga rasmi na Dortmund msimu ujao.

Dortmund walikamilisha mchuano huo wakiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Mahmoud Dahoud kuonyeshwa kadi nyekundu mwishoni mwa kipindi cha pili.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Ruto aonywa asifuate nyayo za Raila kisiasa

Ronaldo aweka rekodi ya ufungaji wa mabao Ulaya