Na MASHIRIKA
FOWADI wa Liverpool, Mohamed Salah na mshambuliaji matata wa timu ya wanawake ya Chelsea, Sam Kerr, ni miongoni mwa wanasoka ambao wamejumuishwa katika orodha ya wawaniaji wa tuzo zitakazotolewa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa Mwanasoka Bora wa Mwaka 2021.
Salah amejumuishwa katika orodha ya wawaniaji wa kiume pamoja na nyota Lionel Messi wa Paris Saint-Germain (PSG) na supastaa wa Bayern Munich, Robert Lewandowski.
Kerr ameteuliwa pamoja na wanasoka wawili mahiri wa Barcelona Jennifer Hermoso na Alexia Putellas katika kitengo cha wanawake.
Washindi watatangazwa wakati wa kutolewa kwa tuzo hizo za Best Fifa Football Awards jijini Zurich, Uswisi mnamo Januari 17, 2022.
Salah kwa sasa ndiye anaongoza orodha ya wafungaji bora wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu kwa mabao 16 baada ya kuambulia nafasi ya pili nyuma ya Harry Kane wa Tottenham Hotspur mnamo 2020-21.
Kwa upande wake, Kerr ambaye ni raia wa Australia, aliongoza Chelsea kuhifadhi ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) mnamo 2021 na kutinga fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).
Washindi wa tuzo hizo hupigiwa kura na makocha wa timu za taifa, manahodha wa timu za taifa, wanahabari na mashabiki.
Lewandowski alishinda tuzo hiyo mnamo 2020 huku Lucy Bronze wa Manchester City na timu ya taifa ya Uingereza akitawazwa mshindi wa kitengo cha wanawake mwaka huo.
Erik Lamela wa Tottenham Hotspur amejumuishwa katika orodha ya wawaniaji wa tuzo ya FIFA Puskas ambayo hutolewa kwa bao zuri zaidi kila mwaka. Bao lake katika gozi la EPL dhidi ya Arsenal mnamo Machi 2021 linapigania tuzo hiyo.
ORODHA YA WAWANIAJI WA TUZO ZA FIFA:
Mchezaji Bora wa Kike:
Mchezaji Bora wa Kiume:
Kocha Bora wa Kike:
Kocha Bora wa Kiume:
Kipa Bora wa Kike:
Kipa Bora wa Kiume:
Tuzo ya Fifa Puskas
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO