• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Sitagura Liverpool hata tukishindwa kufuzu UEFA muhula ujao – Sadio Mane

Sitagura Liverpool hata tukishindwa kufuzu UEFA muhula ujao – Sadio Mane

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI Sadio Mane, 28, amesema atasalia uwanjani Anfield kuvalia jezi za Liverpool hata kama waajiri wake hao watakosa kufuzu kwa gozi la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao wa 2021-22.

Nyota huyo raia wa Senegal amesema hayo baada ya tetesi nyingi kuanza kumhusisha na uwezekano wa kuyoyomea Uhispania kuingia katika sajili rasmi ya Real Madrid ambao wamekuwa wakimhemea kwa misimu miwili iliyopita.

“Nafurahia maisha yangu jijini Merseyside na ninajivunia sana kikosi cha Liverpool. Sioni kabisa uwezekano wowote wa kuagana na klabu hiyo hivi karibuni,” akasema Mane ambaye angali na miaka miwili kwenye mkataba wake wa sasa na Liverpool.

Kufikia sasa, Liverpool wanashikilia nafasi ya saba kwenye msimamo wa jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kwa alama 46, tano zaidi nyuma ya Chelsea wanaofunga mduara wa nne-bora.

Kwa upande wake, kocha Jurgen Klopp amefichua mipango ya kushawishi Liverpool kurefusha mkataba wa Mane katika maagano yatakayomshuhudia sasa akitia mfukoni mshahara wa Sh48 milioni kwa wiki.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa mlo mtamu wa pilau ya kuku na...

Thierry Henry ajiondoa kwenye mitandao ya kijamii...