• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 1:50 PM
Soyaux-Charente anayochezea Mkenya Awuor yazoa ushindi Ligi Kuu Ufaransa

Soyaux-Charente anayochezea Mkenya Awuor yazoa ushindi Ligi Kuu Ufaransa

Na GEOFFREY ANENE

KIPA Lilian Awuor Onyango alikuwa kitini klabu yake mpya ya Soyaux-Charente ikivuna ushindi muhimu kwenye Ligi Kuu ya Soka ya Kinadada nchini Ufaransa baada ya kuchapa wenyeji Dijon 1-0 Jumamosi usiku.

Beki Mfaransa mwenye asili ya Mali, Siga Tandia alifungia Soyaux-Charente bao la pekee na ushindi dakika ya 42 katika mechi hiyo ambayo kipa nambari moja Romane Munich alikuwa michumani.

Soyaux-Charente, ambayo inakamata nafasi ya 10 kwenye ligi hiyo ya timu 12, itazuru viongozi na mabingwa wa zamani Olympique Lyon katika mechi ijayo mnamo Februari 11.

Awuor alijiunga na Soyaux-Charente mnamo Januari 11 kwa kandarasi ya miaka mitatu akitokea mabingwa wa Kenya wa mwaka 2017, 2018 na 2019 na Afrika Mashariki na Kati 2021 Vihiga Queens.

Mechi ya Dijon ilikuwa yake ya pili mfululizo kujumuishwa kwenye kikosi cha siku ya mechi. Alikuwa kitini wakati Soyaux-Charente ililemea Nantes kwa njia ya penalti 4-3 katika Kombe la Ufaransa mnamo Januari 30.

  • Tags

You can share this post!

Rais ahimiza Wakenya kujiandikisha kwa bima ya afya ya...

Lampard aongoza Everton kupepeta Brentford bila huruma...

T L