Na MASHIRIKA
KOCHA mpya wa Everton, Frank Lampard, alianza kazi ugani Goodison Park kwa matao ya juu baada ya kuongoza waajiri wake kukomoa Brentford 4-1 katika raundi ya nne ya Kombe la FA mnamo Jumamosi.
Lampard alirithi mikoba ya Rafael Benitez mnamo Januari 31, 2022, mwaka mmoja baada ya kupigwa kalamu na Chelsea kwa sababu ya msururu wa matokeo duni.
Everton waliwekwa kifua mbele katika dakika ya 31 – hiyo ikiwa mara ya kwanza ambapo wamejiweka kifua mbele katika mechi tangu Oktoba 23, 2021.
Everton walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Yerry Mina aliyeshirikiana na Demarai Gray baada ya kutokea benchi kujaza nafasi ya Ben Godfrey aliyepata jeraha.
Mabao mengine ya Everton yalifumwa wavuni na Richarlison, Mason Holgate na Andros Townsend huku Brentford wakifutiwa machozi na Ivan Toney.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO