• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 10:44 AM
Lampard aongoza Everton kupepeta Brentford bila huruma katika Kombe la FA

Lampard aongoza Everton kupepeta Brentford bila huruma katika Kombe la FA

Na MASHIRIKA

KOCHA mpya wa Everton, Frank Lampard, alianza kazi ugani Goodison Park kwa matao ya juu baada ya kuongoza waajiri wake kukomoa Brentford 4-1 katika raundi ya nne ya Kombe la FA mnamo Jumamosi.

Lampard alirithi mikoba ya Rafael Benitez mnamo Januari 31, 2022, mwaka mmoja baada ya kupigwa kalamu na Chelsea kwa sababu ya msururu wa matokeo duni.

Everton waliwekwa kifua mbele katika dakika ya 31 – hiyo ikiwa mara ya kwanza ambapo wamejiweka kifua mbele katika mechi tangu Oktoba 23, 2021.

Everton walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Yerry Mina aliyeshirikiana na Demarai Gray baada ya kutokea benchi kujaza nafasi ya Ben Godfrey aliyepata jeraha.

Mabao mengine ya Everton yalifumwa wavuni na Richarlison, Mason Holgate na Andros Townsend huku Brentford wakifutiwa machozi na Ivan Toney.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Soyaux-Charente anayochezea Mkenya Awuor yazoa ushindi Ligi...

Senegal wapepeta Misri kwa penalti 4-2 na kutwaa taji la...

T L