• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Sturridge apata hifadhi katika kikosi cha Perth Glory nchini Australia

Sturridge apata hifadhi katika kikosi cha Perth Glory nchini Australia

Na MASHIRIKA

FOWADI wa zamani wa Liverpool na timu ya taifa ya Uingereza, Daniel Sturridge, ametia sani mkataba wa mwaka mmoja na kikosi cha Perth Glory cha Ligi Kuu ya Australia (A-League).

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 hakuwa na klabu tangu aagane na klabu ya Trabzonspor ya Uturuki mnamo Machi 2020.“Ni fursa njema kujaribu changamoto mpya kwingineko,” akasema Sturridge.

“Sturrdige ni miongoni mwa wanasoka stadi zaidi kuwahi kusajiliwa na kikosi cha Perth Glory na katika historia ya A-League,” akasema mmiliki wa kikosi hicho, Tony Sage.

Sturridge alihudumu kambini mwa Liverpool kwa misimu sita ambapo alifunga mabao 67 kutokana na mechi 160 kabla ya kutumwa kwa mkopo katika kikosi cha West Bromwich Albion kwa minajili ya nusu ya kampeni za msimu wa 2017-18.

Aliyoyomea Uturuki bila ada yoyote kuvalia jezi za Trabzonspor mnamo 2019 akiwa mchezaji huru.Mkataba wake wa miaka mitatu na Trabzonspor ulitamatishwa ghafla mnamo Machi 2020 baada ya sogora huyo wa zamani wa Manchester City na Chelsea kupigwa marufuku ya miezi minne kwa kukiuka kanuni zinazodhibiti mchezo wa kamari miongoni mwa wanasoka.

  • Tags

You can share this post!

Ngilu aweka ushirika na NHIF kuwezesha familia 200,000 za...

Bayer Leverkusen yapepeta Celtic bila haya katika Europa...