• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
UDAKU: Pepeta iwake! Szczesny, Marina waimarisha ngoma chumbani kupanua familia

UDAKU: Pepeta iwake! Szczesny, Marina waimarisha ngoma chumbani kupanua familia

IMEKUSANYWA NA CHRIS ADUNGO

KIPA Wojciech Szczesny wa Juventus ya Italia amekiri kuwa yeye na mkewe Marina Luczenko wameanza kutafuta kimalaika cha pili.

Katika mahojiano na gazeti la The Sun wiki hii, Szczesny, 31, alifichua kwamba mimba ya pili ya Marina, 32, iliharibika mwanzoni mwa 2021.

“Alizuru kliniki na akaambiwa yuko sawa. Sasa tunacheza ngoma usiku na mchana na mtajionea matokeo,” akasema mlinda-lango huyo wa Poland.

Szczesny na Marina walifunga pingu za maisha Mei 2016 na wakajaliwa mtoto wa kiume, Liam, mnamo Juni 2018.

Marina ni mwanamuziki na mwanamitindo maarufu mzawa wa Ukraine na raia wa Poland.

Chini ya mojawapo ya picha ambazo hupakia kwenye Instagram, aliandika “Sijachoka na safari ya uzazi. Naponda raha sasa hivi kwa sababu karibuni sitaweza kunywa mvinyo tena.”

Naye Szczesny akajibu: “Hakuna jambo lililo zuri kuliko hili. Tunalenga kupanua familia.”

Mlinda-lango huyo wa zamani wa Brentford, Arsenal na AS Roma alianza kutoka kimapenzi na Marina mnamo 2013 kabla ya kumvisha pete ya uchumba mnamo Julai 2015.

Marina alitumia ziara yake ya hivi majuzi nchini Ukraine kufyatua video rasmi ya kibao chake kipya ‘On My Way’ alichokiachilia Februari 2021.

Nyingi za nyimbo za Marina zinavuma sana katika maeneo mengi ya Mashariki ya bara Ulaya.

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Uunganishaji haramu wa stima waweka wakazi...

KIGODA CHA PWANI: Jinsi mkono wa Joho utakoroga kampeni za...

T L