• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 10:59 AM
Thika Queens bado yalenga kukamilisha kampeni miongoni mwa vikosi nne-bora KWPL

Thika Queens bado yalenga kukamilisha kampeni miongoni mwa vikosi nne-bora KWPL

Na JOHN KIMWERE

MENEJA wa Thika Queens, Glenston Muganda amewataka wachezaji wake wapambane ili kuhakikisha wanashinda mechi zote nne zilizosalia ili kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu ya Kenya ya Wanawake (KWPL) muhula huu.

”Endapo tunalenga kutimiza azma yetu lazima tuwe makini tuhakikishe hatutapoteza alama yoyote kwenye mechi zilizosalia,” alisema na kuongeza anaamini wamekaa vizuri kushinda wapinzani wao wote.

Thika Queens ilianza vibaya kampeni zake na kupoteza tumaini la kutetea ubingwa huo ilioshinda msimu uliyopita.

Kikosi hicho cha kocha, Benta Achieng wikendi hii kitaalika Trans Nzoia Falcons.

Kisha kitakuwa ugenini kucheza na Vihiga Queens ambayo tayari imetwaa taji hilo na mechi ya tatu kitakaribisha Kisumu All Stars.

Mwisho klabu hiyo itaalikwa na Wadadia mjini Mumias. Warembo hao walijiongezea tumaini la kumaliza katika nafasi ya pili walipocharaza Kangemi Starlets kwa mabao 5-0 wikendi iliyopita.

Kwenye jedwali la kipute hicho, Vihiga Queens inaongoza kwa alama 50, nayo Ulinzi Starlets inashikilia nafasi ya pili kwa alama 35, moja mbele ya Thika Queens.

Gaspo Women ni  ya nne kwa alama 33, tatu mbele ya Zetech Sparks.

Thika inajivunia huduma za wachezaji kama Catherine Githae, Hadima Nuru, Wincate Kinyua, Rebecca Okwaro, Fauzia Omar na Salum Tatu kati ya wengine.

  • Tags

You can share this post!

Voliboli: Wawakilishi wa Kenya wawasili nchini Tunisia...

Patrick Jungle na Anne Nyokabi waahidi kuwaletea wakazi wa...

T L