• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:50 AM
Thika Queens yapania kumaliza tatu bora ligi ya KWPL

Thika Queens yapania kumaliza tatu bora ligi ya KWPL

Na JOHN KIMWERE

MABINGWA watetezi kwenye kampeni za Soka la Ligi Kuu ya Wanawake (KWPL), Thika Queens wamepania kukaza buti kuhakikisha wanashinda mechi zote zilizosalia wakilenga kumaliza kati ya tatu bora muhula huu.

Meneja wake, Glenstone Muganga anadokeza kuwa ni kama wamepoteza tumaini la kuhifadhi taji hilo ambapo wanalenga kumaliza kati ya nafasi ya pili na tatu ili kujiweka vizuri kwa kampeni za msimu ujao.

”Kuserma ukweli kampeni za muhula huu zimeshuhudia ushindani mkali,” amesema na kuwataka wachezaji wake zaidi kwenye mechi zijazo. Thika Queens ambayo hunolewa na kocha, Benta Achieng imejikuta kwenye wakati mgumu msimu huu kwa kuzingatia kutokana na mechi 12 imeshinda patashika saba, kutoka nguvu sawa mara mbili na kupoteza mara tatu.

Kwenye ratiba ya kipute hicho Jumapili (10.04.2022) itakuwa katika ardhi ya nyumbani Thika Stadium kualika Bunyore Starlets ambapo lazima ishinde mchezo huo ili kujiongezea tumaini la kutimiza azma yake.

Thika Queens iliyowahi kushinda ligi kuu mara tatu inajivunia huduma za wachezaji kama Wendy Achieng, Catherine Githae, Hadima Nuru, Wincate Kinyua, Rebecca Okwaro, Fauzia Omar na Salum Tatu kati ya wengine.

Kwenye jedwali la mechi hizo Thika inashikilia nafasi ya nne kwa kuzoa alama 23, moja mbele Trans Nzoia Falcons.

You can share this post!

KAULI YA WALLAH BIN WALLAH: Unapokuwa kwenye mapumziko...

Mabilioni kukopwa kugharimia miradi

T L