Na MASHIRIKA
UHISPANIA watakutana na Italia kwenye nusu-fainali za kipute cha Uefa Nations League mwaka huu huku wenyeji Uholanzi wakipepetana na Croatia.
Mechi hizo za hatua ya nne-bora zimeratibiwa kusakatwa kati ya Juni 14-15 huku fainali na mechi nyingine ya kutafuta mshindi nambari tatu na nne ikitandazwa Juni 18. Michuano yote itapigiwa mjini Rotterdam au Enschede.
Uhispania walitandika Italia 2-1 katika nusu-fainali za Nations League mnamo 2021 kabla ya kuzidiwa ujanja na Ufaransa kwa kichapo cha 2-1 kwenye fainali.
Uholanzi nao walitandikwa 1-0 na wenyeji Ureno katika fainali ya kipute hicho mnamo 2019.
DROO YA NUSU-FAINALI ZA NATIONS LEAGUE:
Uholanzi vs Croatia, Juni 14, De Kuip, Rotterdam
Uhispania vs Italia, 15 June, uga wa FC Twente, Enschede
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO