• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Vipusa wa Uswidi kuvaana na Uingereza kwenye nusu-fainali za Euro baada ya kudengua Ubelgiji

Vipusa wa Uswidi kuvaana na Uingereza kwenye nusu-fainali za Euro baada ya kudengua Ubelgiji

Na MASHIRIKA

KOCHA Peter Gerhardsson amesema Uswidi watahitaji “mpango kabambe zaidi” ili kudengua wenyeji Uingereza kwenye nusu-fainali za Euro za wanawake mwaka huu.

Hii ni baada ya warembo wake kulazimishiwa kusubiri hadi dakika ya 92 kubandua Ubelgiji kwa bao 1-0 katika gozi la robo-fainali lililowakutanisha Ijumaa ugani Leigh Sports Village. Ushindi huo uliwakatia Uswidi tiketi ya kuvaana na Uingereza mnamo Julai 26, 2022 uwanjani Bramall Lane.

“Tunatazamia mechi ya kusisimua zaidi. Sawa na wao, nasi hatupigiki kirahisi. Swala kuu ni mbinu tutakazosuka ili kuwatandika. Muhimu ni kuwanyima fursa ya kung’aa mbele ya mashabiki wao wa nyumbani,” akasema Gerhardsson.

Uswidi wanaopigiwa upatu wa kuzoa taji la Euro mwaka huu, walielekeza makombora 33 langoni mwa Ubelgiji ila wakapoteza nafasi nyingi za wazi kabla ya Linda Sembrant kucheka na nyavu sekunde chache kabla ya kipenga cha mwisho kupulizwa.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Maafisa watatu wa polisi wapatikana na hatia ya kumuua...

DOUGLAS MUTUA: Tusisukume wanariadha wetu kusaka uraia wa...

T L