• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 5:50 PM
Vissel Kobe anayochezea Masika yalimwa Kombe la Levain, mashabiki walia kocha afutwe

Vissel Kobe anayochezea Masika yalimwa Kombe la Levain, mashabiki walia kocha afutwe

Na GEOFFREY ANENE

MAMBO ni magumu kambini mwa Vissel Kobe anayochezea Mkenya Ayub Timbe Masika baada ya klabu hiyo kukamilisha michuano mitatu bila ushindi ikichapwa 1-0 na Tokushima Vortis kwenye Kombe la Levain, Jumatano.

Winga huyo mwenye umri wa miaka 28 aliingia uwanjani katika dakika ya 65 kujaza nafasi ya Asahi Masuyama timu hiyo yake ikiwa tayari imefungwa. Atsushi Kawata alifungia wageni Tokushima dakika ya 30.

Kiungo Mjapani mwenye asili ya Nigeria, Joel Chima Fujita alichangia katika bao hilo la pekee alipoiba pasi ya Vissel ndani ya nusu yao na kusuka pasi kwa Yudai Konishi kabla ya Kawata kukamilisha shambulio hilo kwa ustadi. Mabeki wa Tokushima walilinda bao lao hadi kipenga cha mwisho ikiwemo kuzima mashambulizi manne kutoka kwa Timbe.

Matokeo haya yameongeza presha kwa kocha wa Vissel Kobe, Atsuhiro Miura ambaye mashabiki wamekuwa wakitaka atimuliwe.

Mabingwa watetezi FC Tokyo wako juu ya Kundi B kwa alama sita. Watafikisha tisa wakichapa Oita Trinita baadaye leo Jumatano. Vissel Kobe, Tokushima na Oita wamezoa alama tatu kila mmoja, lakini wanatofautiana kwa ubora wa magoli. Oita itaruka juu ya Vissel na Tokushima ikiwa itapata sare ama kushinda Tokyo.

  • Tags

You can share this post!

Kila kaunti kupata daktari wa mifugo atakayesaidia kuondoa...

Hatuogopi yeyote, wanavoliboli wa KPA wajipiga kifua baada...