Na MASHIRIKA
WOLVERHAMPTON Wanderers wamefutilia mbali tetesi kwamba wataagana na Julen Lopetegui na kusisitiza kuwa mkufunzi huyo raia wa Uhispania atasalia kuwa kocha wao msimu ujao wa 2023-24.
Lopetegui alianza kudhibiti mikoba ya Wolves mnamo Novemba 2022 kikosi hicho kikivuta mkia wa jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).
Licha ya kuwaongoza kusalia ligini muhula ujao, kumekuwa na uvumi kwamba mustakabali wake ugani Molineux ulikuwa ukining’inia padogo.
Mnamo Alhamisi, mkurugenzi wa soka kambini mwa Wolves, Matt Hobbs, alisema Lopetegui anafurahia maisha yake kambini mwa Wolves na ametoa hakikisho la kusalia nao hadi atakapofikia malengo ya kikosi.
Lopetegui, 56, amewahi pia kuwanoa masogora wa Real Madrid na timu ya taifa ya Uhispania na amewataka waajiri wake wa sasa kujitolea kadri ya uwezo wao na kumsaidia kusajili wanasoka wa haiba kubwa kwa ajili ya kampeni za msimu ujao wa 2023-24.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO