• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 9:50 AM
Zetech Sparks watuma onyo kwa Thika Queens Kombe la FKF

Zetech Sparks watuma onyo kwa Thika Queens Kombe la FKF

NA AREGE RUTH

KIVUMBI kikali kinatarajiwa katika uwanja wa Ruaraka jijini Nairobi, Jumamosi, wakati Zetech Sparks na Thika Queens watakabana koo katika raundi ya 16 ya Kombe la Wanawake la Shirikisho la Soka nchini (FKF).

Timu hizi ambazo zinashiriki Ligi Kuu ya Wanawake nchini (KWPL), Zetech Berbard Kitolo anasema wameajianda vizuri kuwaondoa Thika kwenye shindano hilo.

“Lengo letu kwenye mechi hiyo ni kushinda na hakuna lingine. Nimewaambia wasichana wangu kwamba huu hautakuwa mchezo rahisi. Tumejipanga vizuri mazoezini lazima Thika wazame,” alisema Kitolo.

“Tumehamishia umakini wetu kwenye mechi hii. Tulipata ushindi dhidi ya Thika Queens katika mechi ya mkondo wa kwanza na tunatumai kufanya vivyo hivyo katika Kombe la Wanawake la FKF,” Nahodha wa Zetech Sparks Puren Alukwe.

Wikendi hii, timu nane zitapambania kuingia kwenye raundi ya nane ya kombe la FKF.

Katika uga uo huo, wanajeshi wa Ulinzi Starlets Ulinzi Starlets watakuwa wenyeji wa Soccer Sister ya Ligi ya Divisheni ya Kwanza (KWPLDV1L).

Mjini Kitale katika uwanja wa Ndura, Royal Starlets itamenyana na Eldoret Falcons. Mombasa Olympic watawafunza Kisumu All Starlets kukuna nazi katika uwanja wa Mbaraki mjini Mombasa.

Nakuru City Queens itagaragazana na Gaspo Women  katika uwanja vya RVIST mjini Nakuru nao Vihiga Queens itawakaribisha  Kisped Queens uwanjani Mumias Sports Complex Mumias.

Jumapili ugani Ruaraka, Kibera Soccer Ladies itamenyana na Falling Waters nao Kahawa Queens watafunga kazi dhidi ya Fortune Ladies

  • Tags

You can share this post!

Dini potovu lasababisha maafa ya wanne

Shule ya Noonkopir yafungwa baadhi ya wanafunzi wakidai...

T L