• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:12 PM
Zetech Sparks yapania kumaliza tatu-bora KWPL

Zetech Sparks yapania kumaliza tatu-bora KWPL

NA JOHN KIMWERE

TIMU ya wanawake ya Zetech Sparks imepania kupambana mwanzo mwisho kuhakikisha inamaliza kati ya nafasi tatu bora kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Soka (KWPL) muhula huu.

Kocha wake, Bernard Kitolo anasema walianza kampeni zao vibaya baada ya mlinda lango namba moja, Valentine Kwaka kupata majareha.

”Kwa sasa tunalenga kukaza buti kwenye mechi tano zilizosalia huku tukipania kumaliza kati ya tatu bora,” alisema na kuongeza kuwa kutoka hapo wataanza maandalizi ya kupigania taji hilo msimu ujao.

Anasema kuwa ujio wa mnyakaji huyo kwenye mechi za mkumbo wa pili umesaidia kikosi hicho kufanya vizuri. Zetech Sparks imezua ushindani wa kuvutia na kusajili ushindi wa mechi sita mfululizo bila kushindwa.

Kocha huyo anasema ana imani kikosi chake kitaendeleza kasi hiyo kitakapokutana na vinara wa kipute hicho Vihiga Queens wikendi hii.

Kwenye msimamo wa kipute hicho, Zetech Sparks inashikilia nafasi ya tano kwa kuzoa alama 30 mbili mbele ya Trans Nzoia Falcons baada ya kushiriki mechi 17 kila moja.

You can share this post!

KASHESHE: Wajigeuza mbogo!

DOMO: Kwa sasa yuko freshi barida!

T L