• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
Ann Kananu aapishwa rasmi kuiongoza Nairobi

Ann Kananu aapishwa rasmi kuiongoza Nairobi

Na MWANDISHI WETU

ANN Kananu ameapishwa leo Jumanne kuwa Gavana wa Tatu wa Kaunti ya Nairobi katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa KICC, leo Jumanne

Hafla hii imetoa fursa ya kupatikana kwa mrithi wa aliyekuwa Gavana Mike Sonko ambaye aliondolewa mamlakani na kura za madiwani ambao walikosa imani na uongozi wake.

Kananu ameahidi kuendelea kuboresha huduma jijini.

“Mimi ni mama na ninaelewa changamoto za wakazi wa Nairobi. Kipindi ambacho nimekuwa kaimu gavana nimesaidia wengi kunyanyuka tena baada ya janga la ugonjwa wa Covid-19 kuyumbisha sekta nyingi,” amesema Kananu.

Ameapishwa baada ya tangazo kuchapishwa rasmi na mwenyekiti wa Kamati ya Mamlaka ya Ofisi ya Gavana aliye pia Katibu wa Kaunti Dkt Jairus Musumba.

Kiapo hicho kimetekelezwa kwa kutii Sheria ya Mamlaka ya Ofisi ya Gavana, 2019, na Kipengee Nambari 74 cha Katiba ya Kenya, 2010.

You can share this post!

SHINA LA UHAI: Saratani ya mapafu: Gharama ya matibabu pigo...

Mwendwa aagizwa ajitenge na soka baada ya kuachiliwa

T L