• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 10:01 PM
Kamket akashifu Raila kupinga ushindi wa Ruto

Kamket akashifu Raila kupinga ushindi wa Ruto

NA FLORAH KOECH

MBUNGE mteule wa Tiaty William Kamket amemkosoa mwaniaji urais wa Azimio Raila Odinga kwa kuwasilisha kesi Mahakama ya Juu kupinga matokeo ya uchaguzi ya urais ya Agosti 9, 2022.

Alipouhudhuria hafla ya kuapishwa kwa Gavana wa tatu kaunti ya Baringo Bw Benjamin Cheboi katika uwanja wa maonyesho ya kilimo wa Kabarnet Alhamisi, Bw Kamket aliyechaguliwa kwa tikiti ya chama cha KANU alimshutumu Odinga kwa kupinga ushindi wa Dkt William Ruto katika kinyang’anyiro cha urais.

Mbunge huyo mwenye siasa kali alisema hakuna wizi wa kura za urais uliofanyika katika eneo lake la uwakilishi bungeni.

Alisema matokeo ya kura yaliyotangazwa na mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC Wafula Chebukati kutoka kituo cha kujumlisha kura cha Chemolingot mnamo Agosti 9 2022 yalikuwa sahihi.

“Matokeo ya kura za urais yaliyotangazwa kutoka Chemolingot ni sahihi,” alisema Kamket.

  • Tags

You can share this post!

Watoto wawili wafa, 19 walazwa baada kula asali yenye sumu

DOUGLAS MUTUA: Wakenya wakome kutazama korti zetu kwa jicho...

T L