• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 5:17 PM
Mkewe Raila amuunga Wanyonyi kugombea ugavana wa Nairobi

Mkewe Raila amuunga Wanyonyi kugombea ugavana wa Nairobi

Na COLLINS OMULO

MKEWE kiongozi wa ODM, Raila Odinga, Bi Ida Odinga, amemuunga mkono mbunge Timothy Wanyonyi (Westlands) kuwania ugavana katika Kaunti ya Nairobi kwa tiketi ya ODM mwaka 2022.

Bi Odinga alimtaja Bw Wanyonyi kuwa kiongozi mwerevu na uwezo kuwahumia wakazi wa kaunti hiyo. Hivyo, Bi Odinga aliwarai wakazi kumuunga mkono Bw Wanyonyi kutimiza ndoto yake.

“Tim (Wanyonyi) amehudumu kama diwani na mbunge kwa mihula miwili. Mnataka aende wapi na tajriba hiyo yote aliyo nayo? Ikiwa ana ndoto, tumsaidieni kuitimiza,” akasema.

“Nawaambieni kwamba ni mtu mzuri na aliyesoma vizuri. Niliwahi kufanya kazi naye pamoja. Ikiwa ni suala linalohitaji ujuzi wa kiakili, ana uwezo mkubwa sana na wa kipekee,” akaongeza.

Alisema hayo Jumamosi alipokuwa akihudumu kwenye hafla ya mahafali kuhitimu katika Taasisi ya Mafunzo ya Upishi ya Kibondeni katika eneo la Muthangari, Westlands, Nairobi.

Bi Odinga alisema hakuna mbunge katika kaunti hiyo aliyefanikiwa kuboresha maisha ya wakazi wake kama Bw Wanyonyi.

  • Tags

You can share this post!

Shujaa yalipiza kisasi dhidi ya Ujerumani kuibuka wafalme...

Mhariri wa zamani wa habari katika NMG afariki

T L