Na KITAVI MUTUA
TASNIA ya uanahabari nchini imepata pigo baada ya kifo cha Bw Gideon Mulaki, aliyehudumu kama Mhariri wa Habari katika shirika la Nation Media Group (NMG), katika miaka ya themanini.
Kulingana na mwanawe, Bw Kyalo Mulaki, babake alikuwa mapumzikoni nyumbani kwake eneo la Ikutha, Kaunti ya Kitui, alipoanza kukumbwa na matatizo ya kupumua.
“Yeye ni miongoni mwa wanahabari wachache waliokamatwa na serikali ya Kanu kutokana na habari alizoandika kuukosoa utawala huo,” akasema Bw Wangethi Mwangi, aliyehudumu kwa wakati mmoja kama Mhariri Mkuu katika NMG.