• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Mhariri wa zamani wa habari katika NMG afariki

Mhariri wa zamani wa habari katika NMG afariki

Na KITAVI MUTUA

TASNIA ya uanahabari nchini imepata pigo baada ya kifo cha Bw Gideon Mulaki, aliyehudumu kama Mhariri wa Habari katika shirika la Nation Media Group (NMG), katika miaka ya themanini.

Kulingana na mwanawe, Bw Kyalo Mulaki, babake alikuwa mapumzikoni nyumbani kwake eneo la Ikutha, Kaunti ya Kitui, alipoanza kukumbwa na matatizo ya kupumua.

“Yeye ni miongoni mwa wanahabari wachache waliokamatwa na serikali ya Kanu kutokana na habari alizoandika kuukosoa utawala huo,” akasema Bw Wangethi Mwangi, aliyehudumu kwa wakati mmoja kama Mhariri Mkuu katika NMG.

You can share this post!

Mkewe Raila amuunga Wanyonyi kugombea ugavana wa Nairobi

Nassir na Shahbal wabishania ‘Baba’

T L