Na CHARLES WASONGA
MIPANGO ya Seneta wa Kakamega Cleophas Malala kuwalazimisha vinara wa One Kenya Alliance (OKA), Musalia Mudavadi na Moses Wetang’ula kuunga mkono azma ya urais ya Naibu Rais William Ruto ilifichuka Ijumaa.
Ufichuzi huo ulitolewa na Katibu Mkuu wa Ford Kenya Chris Wamalwa aliyesema Bw Malala alitaka kutafanya hivyo wakati wa finali za mchuano wa kombe la Cleo Malalah Challenge Cup katika uwanja wa michezo wa Mumias Complex, mjini Mumias.
Bw Wamalwa alisema kuwa Bw Malala alikuwa amemshauri Dkt Ruto kufika katika uwanja huo akiwa amechelewa baada ya Mudavadi na Wetang’ula kufika. Ni hapo ambapo yeye Malala angetangaza kuwa OKA itamuunga mkono Dkt Ruto.
“Hatukuenda Mumias kwa sababu Seneta Malala alikuwa amewahadaa viongozi wetu Mheshimiwa Mudavadi na Mheshimiwa Wetang’ula. Alikuwa amepanga njama na William Ruto kuaibisha viongozi wetu kwa kutangaza kuwa wanamuunga mkono Dkt Ruto,
Hata yaliibuka baada ya Mbw Mudavadi na Wetang’ula kufutulia mbali mipango yao ya awali ya kuhudhuria fainali hiyo licha ya kualikwa kuwa wageni waheshimiwa katika shughuli hiyo.