• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 5:50 AM
Mung’aro ajisifu ndiye kipenzi cha wapigakura wa Kilifi

Mung’aro ajisifu ndiye kipenzi cha wapigakura wa Kilifi

NA ALEX KALAMA

MWANIAJI WA KITI cha ugavana wa Kilifi kupitia chama cha ODM, Bw Gideon Mung’aro, amepinga dai kwamba wagombeaji wengine wa kiti hicho kwenye muungano wa Azimio la Umoja One Kenya katika kaunti hiyo wana umaarufu zaidi kumzidi.

Bw Mung’aro amesema kuwa yeye ndio mwenye umaarufu zaidi kwenye kaunti hiyo baada ya kuwa mwanasiasa wa muda mrefu katika sehemu hiyo.

“Wengine walikuja juzi lakini mimi nimekuwa kiongozi katika Kilifi kaunti jina langu halitaki kwenda uambiwe Mung’aro ndiye huyu kila mtu nafikiri wengi labda ni watoto wa juzi. Wengi wananijua kama hawajamuona Mung’aro lakini jina wamelisikia. Kwa hivyo nafikiri kuwa sina wasiwasi na hilo tutaongea na wananchi na sina hofu,nilivyoongoza katika upande wa mrengo wa ODM wakati ule na hata wa azimio la Umoja one Kenya pia nitaongoza,” alisema Bw Mung’aro.

Hata hivyo, kiongozi huyo amewahakikishia wananchi wa kaunti hiyo kuwa atafanya uamuzi bora wakati wa kumchagua naibu gavana wa kaunti hiyo.

“Hili ni suala ambalo linatarajiwa na nimeona kweli kwa vyombo vya habari kila mtu anapiga upatu upande wake hiyo ina maana kwamba mrengo wetu una ushawishi mkubwa kila mtu anataka kujihusisha nao. Mimi nataka ni wahakikishie watu wa Kilifi kwamba tuko na wakati mpaka tarehe kumi na sita mwezi huu na mwenyezi mungu akipenda tutakuwa na jawabu ambalo litafurahisha watu wote wa Kilifi,” alisema Bw Mung’aro.

Haya yamejiri zikiwa zimebaki siku kumi pekee kabla ya wawaniaji wa urais na wale wa ugavana nchini kupeleka majina ya wagombea wenza ama manaibu wao kwa tume Huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC.

  • Tags

You can share this post!

Sheikh akataa kutoka Kamiti

Timamy aapa kurejesha tamasha za kitamaduni

T L