NA KENYA NEWS AGENCY
MWAKILISHI wa Wanawake katika Kaunti ya Makueni, Bi Rose Museo, ametangaza kwamba atatetea kiti chake kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti.
Bi Museo, ambaye awali alikuwa akilenga kuwania ugavana, alisema alibadilisha msimamo wake baada ya kufanya mashauriano na kiongozi wa chama cha Wiper, Bw Kalonzo Musyoka.