NA SAMWEL OWINO
SENETA wa Kaunti ya Siaya Oburu Oginga na Mbunge Mwakilishi wa Jinsia ya Kike wa Kaunti ya Siaya Christine Ombaka sasa wanataka Gavana James Orengo na naibu wake William Oduol wasuluhishe tofauti baina yao.
Wawili hao wamekuwa na mvutano wa muda mrefu na hata imefikia hatua ambapo baadhi ya madiwani wanataka kupiga kura ya kumwondoa Bw Oduol katika nafasi hiyo.