• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
Ongwae aongoza viongozi kadhaa kujiunga na Ruto

Ongwae aongoza viongozi kadhaa kujiunga na Ruto

NA RUTH MBULA

ALIYEKUWA Gavana wa Kisii James Ongwae na wanasiasa wengine kutoka eneo la Gusii waliopoteza katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9 wamegura muungano wa Azimio la Umoja One Kenya na kujiunga na Kenya Kwanza.

Ijumaa asubuhi, viongozi hao kutoka kaunti za Kisii na Nyamira walikutana na Rais mteule William Ruto katika makazi yake mtaani Karen, Nairobi katika kile kilichoonekana kama mwanzo wa ushirikiano kati yao na serikali mpya.

Wengine walioandama na Bw Ongwae ni; aliyekuwa Waziri Msaidizi wa Uchukuzi Chris Obure, aliyekuwa Mwakilishi wa Kike Kisii Janet Ong’era, wabunge wa zamani Jimmy Angwenyi (Kitutu Chache Kaskazini), Richard Tong’i (Nyaribari Chache), Ben Momanyi (Borabu), Manson Nyamweya ( Mugirango Kusini) na Zadock Ogutu (Bomachoge Borabu).
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Abagusii Araka Matundura pia alikuwepo.

  • Tags

You can share this post!

Elizabeth II alipata umalkia akiwa ziara nchini Kenya

Uhusiano wa Malkia Elizabeth, ‘pembe za ndovu’...

T L