NA ALEX NJERU
MWANIAJI wa Useneta Kaunti ya Tharaka-Nithi, Bw Samuel Ragwa (pichani) ambaye alipoteza kwenye mchujo wa UDA wiki jana, ametangaza kuwa sasa atawania kama mwaniaji huru kwenye uchaguzi wa Agosti 9.
Bw Ragwa alisema hawezi kukata rufaa kuhusu uteuzi huo aliodai ulijaa udanganyifu na kuhujumu demokrasia.
Alibwagwa na Diwani wa Mukothima, Mwenda Gataya aliyepata kura 40,746 .