NA MARY WANGARI
ITAMGHARIMU kinara wa Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga, zaidi ya Sh1.5 milioni kuwasilisha kesi ya kupinga matokeo ya urais katika Mahakama ya Juu.
Kiongozi wa ODM anatazamiwa kuwasilisha kesi ya kupinga ushindi wa mpinzani wake William Ruto aliyetangazwa na IEBC Jumatatu kama Rais Mteule.