NA BRIAN OCHARO
USHINDI wa Seneta wa Kwale, Boy Issa Juma katika uchaguzi uliokamilika umetiliwa shaka baada ya mpinzani wake, Salim Ali Mwadumbo kutaka uchaguzi wake ubatilishwe kwa sababu ya dosari.
Bw Juma alifanikiwa kutetea kiti chake baada ya kuzoa kura 52,772 katika kinyang’anyiro kilichovutia wagombeaji tisa.