• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 7:02 PM
Wanga alia yumo hatarini mchujo ukikaribia

Wanga alia yumo hatarini mchujo ukikaribia

NA GEORGE ODIWUOR

MWAKILISHI wa Kike katika Kaunti ya Homa Bay, Bi Gladys Wanga, ameiomba Wizara ya Usalama wa Ndani kumpa ulinzi zaidi, akihofia huenda akashambuliwa wakati huu mchujo wa chama cha ODM unapokaribia.

Bi Wanga ambaye ananuia kuwania ugavana, ameisihi wizara kuangazia anachosema kuwa vitisho na kuingizwa baridi kwa wanasiasa wanawake nchini.

Haya yamejiri huku wagombea wakiimarisha kampeni za mchujo wa wawaniaji utakaofanyika Aprili.

Alihimiza mashirika ya usalama kukabiliana na wanaojaribu kutumia mbinu zisizo za haki kuwasukuma wanasiasa wanawake nje ya uchaguzi wa Agosti 9.

Pia anataka wafuasi wa wawaniaji wa kike kulindwa akidai baadhi wanashinikizwa kuwaunga mkono wagombea fulani.

Kaunti ya Homa Bay huwa inagubikwa na ghasia hasa nyakati za msimu wa siasa.

Hata hivyo, kwa sasa, wagombea wameendelea kuuza sera zao katika juhudi za kukuza umaarufu wao.

“Kundi la wanaume wenye ajenda fiche wameungana kunishambulia. Mimi ndiye suala la mjadala katika mikutano yote ya kampeni na baadhi ya mambo wanayosema, yanalenga kunidhuru bila kunufaisha jamii chochote,” alilalama mwakilishi huyo.

You can share this post!

AS Monaco waaibisha PSG katika Ligi Kuu ya Ufaransa

Asha Hussein aimarisha kampeni zake kutetea kiti chake...

T L