• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 5:40 PM
Wazee watatizika mitambo ikishindwa kunasa alama za vidole

Wazee watatizika mitambo ikishindwa kunasa alama za vidole

NA WAANDISHI WETU

BAADHI ya wazee, akiwemo mamake Mbunge wa Malindi, Bi Aisha Jumwa, jana Jumanne walikumbwa na changamoto kupiga kura wakati mashine za kutambua wapigakura, almaarufu KIEMS, ziliposhindwa kunasa alama za vidole vyao.

Bi Jumwa, ambaye ni mgombeaji ugavana Kilifi kupitia UDA, alikuwa wa kwanza kupiga kura katika kituo cha shule ya upili ya wavulana ya Kakuyuni.

Mamake ambaye alimfuata, alitatizika kutambuliwa kwa vidole ikalazimu maafisa wa uchaguzi kutafuta mbinu nyingine za kumtambua.Katika Kaunti ya Kwale, Taifa Leo iliwapata baadhi ya wazee wakitumia limau na mawe kusafisha mikono yao.

Walipohojiwa, walisema walikuwa wameambiwa wakasafishe mikono kwa vile mitambo ya KIEMS haingewatambua kwa vidole.

Katika eneobunge la Jomvu, Kaunti ya Mombasa, Bi Jumwa Thoya, 79, alilalamika kuwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilishindwa kumtambua ilhali amepiga kura katika kituo hicho cha shule ya msingi ya Amani kwenye chaguzi karibu zote zilizopita.

Maafisa wa IEBC walimwambia kuwa, alifaa kupiga kura Kwale na zaidi ya hayo, alama za vidole vyake hazingesomeka kwa sababu ya uzee.

“Nilithibitisha nimesajiliwa hapa kupiga kura. Huu ni utani? Sitoki hapa hadi nichague wagombeaji ninaowataka,” akasema.

Katika eneobunge la Changamwe, Kaunti ya Mombasa, mzee wa umri wa miaka 85 alijitokeza kupiga kura licha ya kufanyiwa upasuaji wa figo siku chache zilizopita.

Bw Shikari Kabani Mwambua aliwasili akisaidiwa na mjukuu wake kabla ya kuelekea katika hospitali ya rufaa ya Pwani kwa matibabu ya kusafisha figo.

“Ninawashukuru maafisa wa IEBC kwa kuwa wamenisaidia. Hali yangu si nzuri ila nimeamua nije ili nitekeleze wajibu wangu wa kidemokrasia,” alisema Bw Mwambua.

Kwingineko, mgombeaji ubunge wa Mvita kwa tikiti ya UDA, Bw Omar Shallo, Jumanne alizuiliwa katika kituo cha polisi cha Makupa baada ya makabiliano kuzuka katika kituo cha kura cha ukumbi wa Tudor Village.

Afisa wa NYS alijeruhiwa katika fujo hizo akakimbizwa hospitalini.

  • Tags

You can share this post!

ODM yashuku hila ugavana ukiahirishwa

Bournemouth wasajili kipa mzoefu, Murara Neto, kutoka...

T L