• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Manuel Locatelli wa Italia ajiunga na Juventus

Manuel Locatelli wa Italia ajiunga na Juventus

Na MASHIRIKA

KIUNGO matata raia wa Italia, Manuel Locatelli, amejiunga rasmi na Juventus kwa mkopo wa miaka miwili kutoka Sassuolo.

Locatelli, 23, alikuwa sehemu ya kikosi kilichoshindia Italia ubingwa wa Euro 2020 mnamo Julai baada ya kufunga mabao mawili katika mechi tano na akaletwa uwanjani mwishoni mwa kipindi cha pili kwenye fainali dhidi ya Uingereza.

Kwa mujibu wa kandarasi ya Locatelli, Juventus watakuwa radhi kumpa kandarasi ya kudumu ya miaka mitatu ambayo itagharimu Sh4.9 bilioni kuanzia Juni 2023.

Locatelli ambaye pia amewahi kuchezea AC Milan, aliingia katika sajili rasmi ya Sassuolo mnamo 2018 na amekuwa akimezewa pakubwa na Arsenal pamoja na Liverpool.

Chini ya kocha Andrea Pirlo aliyepigwa kalamu mnamo Mei 2021, Juventus walikosa kutwaa taji la Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mara ya kwanza tangu 2012 na wakaambulia nafasi ya nne jedwalini.

Hatua hiyo iliwashuhudia wakiajiri upya kocha Massimiliano Allegri ambaye atawaongoza kuanza kampeni za msimu wa 2021-22 Serie A dhidi ya Udinese mnamo Agosti 22, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

 

  • Tags

You can share this post!

Kipa Aaron Ramsdale pua na mdomo kuingia katika sajili ya...

Batshuayi arefusha mkataba wake kambini na Chelsea na kutua...