• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Alice Ng’ang’a aongoza maandamano makali kulaani matamshi ya Gakuyo

Alice Ng’ang’a aongoza maandamano makali kulaani matamshi ya Gakuyo

Na LAWRENCE ONGARO

SIASA za eneobunge la Thika zimeanza kushika kasi huku mahasimu wawili Alice Ng’ang’a na Askofu David Kariuki Gakuyo, wakirushiana cheche za maneno.

Mnamo Jumanne, aliyekuwa mbunge wa Thika Bi Alice Ng’ang’a, aliongoza wanawake zaidi ya 200 kukashifu matamshi ya Askofu David Gakuyo, aliyoyatamka hivi majuzi ambapo inadaiwa alimdhalilisha diwani maalum mjini Thika.

Wanawake hao walidai ya kwamba Askofu huyo hana heshima kwa akina mama.

Inadaiwa alikashifu mavazi yake aliyovaa diwani huyo.

Bi Ng’ang’a naye aliandamana na viongozi kadha wa kike kama aliyekuwa mbunge wa Ruiru Esther Gathogo na Mwakilishi wa Wanawake Bi Gathoni wa Muchomba, pamoja na wawaniaji kadhaa wa viti vya kisiasa. Pia wanawake wengine walijitokeza kuwaunga mkono.

Aliyekuwa mbunge wa Thika Bi Alice Ng’ang’a, aliongoza wanawake zaidi ya 200 kukashifu matamshi ya Askofu David Gakuyo. PICHA | LAWRENCE ONGARO

Bi Ng’ang’a alidai kuwa Askofu Gakuyo hakuwa na heshima kwa matamshi yake ya hivi majuzi, na kwa hivyo “alidunisha heshima ya akina mama.”

“Sisi akina mama tumekasirishwa kabisa na matamshi ya Askofu Gakuyo, na kwa hivyo tunalaani maneno yake ya kutudharau,” alifafanua Bi Ng’ang’a alipokuwa akihutubia wanawake hao mjini Thika.

Wanawake hao walihutubia wakazi wa Thika waliofika kusikiliza hotuba yao ya malalamiko.

Baadaye waliandamana hadi kituo cha polisi cha Thika ili kuwasilisha maandishi waliotaka yafuatwe ili kutunza heshima ya wanawake.

Naye Askofu mkuu wa kanisa la The Calvary Chosen Church mjini Thika, David Kariuki Gakuyo, alijitetea vikali akisema matamshi yake hayakuwa na ubaya wowote kwa sababu kiongozi wa kike aliyelenga hakuvalia ifaavyo.

Hata hivyo, alitaja malalamiko ya viongozi hao kama ya kisiasa ili ukweli uepukwe.

“Mimi sina ubaya na yeyote lakini yeyote anayetaka kupiga siasa afanye hivyo kwa njia ifaayo wala si kwa njia ya kujitakia makuu,” alijitetea Askofu huyo.

Alisema yeye kama mchungaji hana ubaya na wanawake kwani anawaheshimu sana kwa hivyo “waache siasa za kuviziana.”

Askofu Gakuyo na Bi Ng’ang’a wanawania kiti cha ubunge cha Thika huku ikidaiwa uchaguzi huo wa Agosti 9, 2022, utakuwa ni wa kukata na shoka kwani kila mmoja ana wafuasi wake wengi.

  • Tags

You can share this post!

Nigeria wazamisha Misri katika mechi ya Kundi D kwenye AFCON

Familia kortini kupinga hatua ya kuwahamisha

T L