NA CHARLES ONGADI
BONDIA Mwinyi Kombo Faki wa klabu ya Kongowea inayoshiriki Ligi Kuu ya Ndondi Nchini anaendeleza mazoezi makali akilenga kuitwa katika timu ya taifa.
Kombo ameimarisha mazoezi yake katika ukumbi wa klabu ya Kongowea akishirikiana na mwenzake Anne ‘Waiguru’ Wanjiru ambaye tayari yuko katika timu ya taifa ya akina dada.
“Lengo langu mwaka huu ni kuwakilisha taifa,” akasema Kombo anayecheza uzito wa unyoya.