Na MARGARET MAINA
KUANDAA: Dakika 20
Mapishi: Dakika 60
Walaji : 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Washa ovena weka nyuzi joto 350° F
Chukua bakuli weka unga, sukari, baking powder, baking soda, mdalasini, nutmeg, na chumvi kisha changanya vizuri. Weka pembeni.
Chukua bakuli ingine weka mayai, siagi, vanilla na flaked coconut halafu koroga mpaka viwe laini kabisa.
Mchanganyiko wenye mayai mwagia kwenye unga kisha koroga mpaka uone vimechanganyikana vizuri.
Chukua karoti ulizoziandaa ukazikwangua uzitie kwenye mchanganyiko ule wa keki. Koroga vizuri sana.
Chukua chombo unachotumia kuokea keki yako ukipake siagi.
Chukua mchanganyiko wa keki mwagia kwenye chombo hicho kisha weka kwenye ovena.
Dakika 45 zikipita, funua angalia kama keki imeiva. Chukua kisu ukidungie katikati ya keki, kikitoka kikavu basi keki itakuwa imeiva. Ikiwa bado, irudishe kwenye ovena ili iive jinsi inavyotakikana.
Baada ya muda mchache chakula chako kitakuwa tayari kuliwa.