• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 9:50 AM
Serikali yajiondoa kwa biashara ya hoteli

Serikali yajiondoa kwa biashara ya hoteli

Na BERNARDINE MUTANU

Serikali imeanza mikakati ya kuuza hisa zake katika hoteli kubwa za kifahari nchini.

Hoteli hizo ni InterContinental, Hilton na Mountain Lodge. Tume ya kubinafsisha inatafuta wataalamu kufanyia hoteli hizo uchunguzi na hoteli zingine ndogo kwa lengo la kuziuzia wawekezaji wa kibinafsi.

Tume hiyo hata hivyo haikuelezea pesa inazotarajia kupata kutoka kwa mauzo ya hoteli hizo.

Wachunguzi hao wanatarajiwa kubainisha hali ya kifedha ya hoteli hizo na kutayarisha kandarasi ikiwemo ni pamoja na mikataba ya kuhawalisha hisa hizo.

Mauzo ya hoteli hizo yalitangazwa mara ya kwanza 2011 kama sehemu ya kuimarisha mapato ya serikali.

Serikali ina hisa 40.57 katika Mahoteli ya Intercontinental yanayomiliki Hoteli ya Hilton.

Inalenga kutoa asilimia 33.83 ya hisa zake kwa Kenya Hotel Properties Limited ambayo inasimamia InterContinental na asilimi 39.11 inazomiliki katika Hoteli ya Mountain Lodge, chini ya usimamizi wa TPS Serena.

You can share this post!

Je, maji haya yatapunguza gharama ya umeme?

Ni faida tu kwa benki ya Equity

adminleo