• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 9:50 AM
Homeboyz wazidi kutesa kwenye Raga ya Kitaifa

Homeboyz wazidi kutesa kwenye Raga ya Kitaifa

Na GEOFFREY ANENE

VIONGOZI Homeboyz wameacha mpinzani wa karibu Mwamba kwa alama sita kwenye Raga ya Kitaifa ya wachezaji saba kila upande, huku KCB, Kabras Sugar, Nondies, Masinde Muliro (MMUST), Blak Blad na Kisii zikiimarika baada ya Sepetuka Sevens, Julai 28, 2018.

Mabingwa wa duru za Prinsloo na Sepetuka, Homeboyz wana alama 44. Nambari mbili Mwamba wamezoa alama 38. Nafasi tatu zinazofuata zinashikiliwa na KCB (alama 32), Impala Saracens (27) na Kabras (23). Impala imerukwa na KCB. Nakuru inasalia ya sita kwa alama 22, mbili mbele ya Nondies, ambayo imepaa nafasi tano. Menengai Oilers imekwamilia nafasi ya nane kwa alama 18, mbili zaidi ya Kenya Harlquin, ambayo imeteremka nafasi nne. Mean Machine imeshuka nafasi moja hadi nambari 10 kwa alama 13. MMUST inashikilia nafasi ya 11 kwa alama 12. Makundi ya duru ijayo ya Kabeberi Sevens itakayofanyika Agosti 18-19 mjini Machakos, imefanywa.

Droo ya Kabeberi Sevens (2018):

Kundi A – Homeboyz, Nakuru, Oilers, Strathmore;

Kundi B – Mwamba, Impala, Blak Blad, Kisumu;

Kundi C – KCB, MMUST, Kisii, Harlequin;

Kundi D – Nondies, Kabras, Machine, Northern Suburbs.

Matokeo ya Sepetuka Sevens (2018):

Julai 29

Fainali – Homeboyz na Mwamba; Mechi ya kuamua nambari 3 na 4 – KCB 15-7 Nondies; Nusufainali – Homeboyz 12-5 KCB, Mwamba 24-12 Nondies; Fainali ya nambari 5/6 – MMUST 12-21 Kabras Sugar; Nusufainali ya nambari 5 hadi 8 –Impala Saracens 14-19 MMUST, Nakuru 5-21 Kabras Sugar; Robofainali – Homeboyz 29-0 Kabras Sugar, KCB 22-8 Nakuru, Mwamba 12-10 MMUST, Impala Saracens 14-17 Nondies; Fainali ya Challenge Trophy – Menengai Oilers 19-14 Blak Blad; Nusufainali ya Challenge Trophy – Menengai Oilers 22-14 Kisii, Blak Blad 27-12 Mean Machine; Robofainali ya Challenge Trophy – Menengai Oilers 24-0 Kisumu, Kisii 48-0 Catholic Monks, Strathmore Leos 12-21 Mean Machine, Blak Blad 14-12 Kenya Harlequins; Fainali ya nambari 13/14 – Kenya Harlequins 45-0 Kisumu; Nusufainali ya nambari 13 hadi 16 – Kisumu 31-12 Catholic Monks, Kenya Harlequins 31-19 Strathmore Leos.

Julai 28

Mechi za makundi – Nakuru 43-0 Catholic Monks, Impala Saracens 17-5 Blak Blad, Kabras Sugar 24-14 Strathmore Leos, Mwamba 38-0 Kisumu, Menengai Oilers 24-7 Mean Machine, Homeboyz 33-17 MMUST, Nondies 12-0 Kenya Harlequins, KCB 29-0 Kisii, Nakuru 26-19 Blak Blad, Impala Saracens 24-7 Catholic Monks, Kabras Sugar 7-5 Kisumu, Mwamba 14-12 Strathmore Leos, Menengai Oliers 7-10 MMUST, Homeboyz 27-5 Mean Machine, Kisii 28-0 Kenya Harlequins, KCB 15-10 Nondies, Catholic Monks 7-26 Blak Blad, Impala Saracens 26-7 Nakuru, Strathmore Leos 17-0 Kisumu, Mwamba 19-7 Kabras Sugar, Mean Machine 12-24 MMUST, Homeboyz 31-10 Menengai Oilers, Nondies 29-5 Kisii, KCB 12-12 Kenya Harlequins.

You can share this post!

Wazito wasisitiza watasalia ligini

ULIMBWENDE: Mbinu 8 bora za kulainisha ngozi

adminleo