• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Mchuuzi aliyelima wenzake mangumi asamehewa

Mchuuzi aliyelima wenzake mangumi asamehewa

Na RICHARD MUNGUTI

MCHUUZI katika eneo la River Road, jijini Nairobi anayekabiliwa na shtaka la kuwapiga wachuuzi wenzake wawili amesamehewa na mahakama kwa kuwalima makonde.

Edith Breda aliondolewa lawama na hakimu mkuu mahakama ya Milimani Lucas Onyina na kushauriwa “asirudi kuwachangamkia anapotofautiana nao kwa masumbwi.”

Mahakama ilitamatisha kesi dhidi ya Edith baada ya mlalamishi Bi Mercy Kathure kumsamehe.

Edith alieleza korti wameafikiana na walalamishi wamwondolee lawama.

Edith aliyejitetea mbele ya hakimu alisema “walileta mchezo kazini nikawacharaza. Lakini sasa tumekubali yaishe na wanisamehe.”

Mercy Kathure, mmoja wa walalamishi waliopigwa na kujeruhiwa na Edith alijieleza mbele ya Bw Onyina na kusema “hataki kuendelea na kesi.”

Mercy aliyekuwa shahidi katika kesi nyingine alisema “ataenda kuitamatisha pia.”

“Nenda ukaondoe malalamishi katika kesi hiyo nyingine kisha urudi umsamehe Edith,” Onyina alimweleza Mercy.

Edith anakabiliwa na shtaka la kumpiga na kumjeruhi Mercy mnamo Machi 13, 2023 katika barabara ya Latema eneo la River Road, Kaunti ya Nairobi.

  • Tags

You can share this post!

DPP, DCI na IG wakunja mkia katika kesi ya Matiang’i

Wanafunzi 8,000 wanufaika na hundi za basari Starehe

T L