• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 9:50 AM
Nakuru kuwa jiji endapo Rais ataidhinisha uamuzi wa maseneta

Nakuru kuwa jiji endapo Rais ataidhinisha uamuzi wa maseneta

Na CHARLES WASONGA

MJI wa Nakuru sasa utapandishwa hadhi na kuwa jiji la nne nchini endapo Rais Uhuru Kenyatta ataidhinisha uamuzi wa maseneta kupitisha ombi la kutaka upandishwe ngazi.

Maseneta wote waliohudhuria kikao cha Alhamisi alasiri waliunga mkono hoja iliyowasilisha na Kamati ya Ugatuzi ambayo ilipitisha ombi hilo.

Hoja hiyo ilipitishwa licha ya madai kutoka kwa baadhi ya viongozi wa kaunti ya Nakuru kwamba serikali hiyo aliwatupa watoto chokoraa katika msitu wa Chemususu kusudi mji wa Nakuru upata hadhi hiyo mpya.

Maseneta wanachama wa Kamati hiyo, inayoongozwa na Seneta wa Homa Bay Moses Kajwang, walisema licha ya kutolewa kwa madai hayo, mji wa Nakuru umetimiza masharti yote ya kupindisha hadhi kuwa jiji.

“Tumetembelea mji wa Nakuru na kugundua kuwa umetimiza sifa zote zinazohitajika kwake kupandishwa hadhi. Kwa hivyo, kamati yangu imeidhinisha kuwa mji wa Nakuru upewe nafasi ya kuwa jiji,” akasema Bw Kajwang’.

Kwa hivyo, sasa Rais Kenyatta atahitajika kuupa mji wa Nakuru hati ya kupanda cheo kwa mujibu wa sehemu ya 7 ya Sheria kuhusu Miji na Majiji.

You can share this post!

Kocha Ronald Koeman kuendelea kudhibiti mikoba ya Barcelona

ICJ, Linda Katiba zashambulia Uhuru