• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 3:33 PM
Stoke City warefusha mkataba wa kiungo Obi Mikel kwa mwaka mmoja zaidi

Stoke City warefusha mkataba wa kiungo Obi Mikel kwa mwaka mmoja zaidi

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

STOKE City wamemwachilia kiungo Jordan Cousins na kurefusha mikataba ya wanasoka John Obi Mikel na James Chester kwa mwaka mmoja zaidi kwenye Ligi ya Daraja la Kwanza nchini Uingereza (Championship).

Cousins, 27, aliwajibishwa na Stoke City mara 45 katika kipindi cha misimu miwili iliyopita.Mikel ambaye ni raia wa Nigeria, aliwahi kusaidia Chelsea ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kushinda ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) na mataji mawili ya EPL.

Sogora huyo mwenye umri wa miaka 34 amekuwa nahodha wa Stoke City kwa kipindi cha msimu mmoja uliopita.Alichezeshwa na Stoke City almaarufu ‘Potters’ mara 41 katika msimu wa 2020-21 baada ya kuingia katika sajili rasmi ya kikosi hicho kutoka Trabzonspor ya Uturuki.

Kwa upande wake, Chester ambaye amewahi kuchezea Aston Villa, aliwajibishwa na Stoke City mara 33.

 

  • Tags

You can share this post!

Kipa Sergio Romero kati ya wachezaji wanane ambao...

Gerrard na Benitez kati ya wakufunzi sita wanaomezea mate...