• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Demu aamua wanaommezea mate wafanye ‘interview’

Demu aamua wanaommezea mate wafanye ‘interview’

NA JANET KAVUNGA

SHANZU, MOMBASA

MWANADADA wa hapa aliwaita makalameni wawili waliokuwa wakimmezea mate kwa kikao na kutaka kila mmoja amweleze kwa nini anampenda kabla ya kufanya uamuzi.

Demu alichukua hatua hiyo majamaa hao ambao ni marafiki walipogombana kila mmoja akilaumu mwenzake kwa kunyemelea mpenzi wake.

Binti wa watu alicheza kama yeye kwa kuwaleta kwenye meza na kutaka kila mmoja kueleza mbele ya mwenzake sababu ya kumpenda.

Jamaa wa kwanza alisema anampenda kwa sababu ni mrembo na wa pili akasema angetaka kumuoa.

Huyo wa pili aliongeza kuwa angetaka mtu mcha Mungu kama demu huyo kuwa mkewe.

Demu alikubaliana naye na kumwambia jamaa wa kwanza alianguka mtihani.

  • Tags

You can share this post!

Makabila makubwa yajinyakulia nafasi nyingi za ajira katika...

Maeneo bunge yasiyo na idadi tosha ya watu kumezwa

T L