• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:42 PM
Jombi aduwaa binti kumrushia mistari motomoto ya mapenzi

Jombi aduwaa binti kumrushia mistari motomoto ya mapenzi

NA JANET KAVUNGA

BAMBURI, MOMBASA

BAROBARO aliyefika eneo hili kujivinjari, alibaki mdomo wazi kipusa anayefanya kazi katika hoteli aliyokuwa akiishi alipomrushia mistari ya mapenzi bila hofu ya kukataliwa.

Jamaa alikuwa ametulia mezani akibugia kinywaji mwanadada huyo alipomjia, akamwamkua kisha akampa ujumbe ambao ulimshangaza.

“Kwa kweli siwezi nikaendelea kuficha yaliyo moyoni. Sijui utakavyolichukua hili lakini ujue nilikutamani tangu siku ya kwanza ulipofika kwenye hoteli hii. Uliteka moyo wangu na siwezi kuvumilia na nimeamua kukufungulia moyo wangu,” demu alimweleza jamaa ambaye hakuamini maneno aliyosikia.

“Asante,” jamaa alisema na demu ambaye alikuwa kazini akaondoka huku akiacha kadi iliyokuwa na nambari yake ya simu na ujumbe uliosema: “Nipigie simu baada ya kazi tuzungumze zaidi. Usinivunje moyo tafadhali.”

  • Tags

You can share this post!

Ushauri nasaha kwa wanafunzi wa shule Nakuru kufuatia kifo...

Ben 10 wanavyosaka mapenzi ya kina mama mitandaoni,...

T L