NA JANET KAVUNGA
MALINDI MJINI
JOMBI wa hapa alijuta kukutana na mpenzi wake wa zamani, mkewe alipopata habari na kumfokea vikali.
Jamaa alisema alikutana na ex wake katika mkahawa, wakasalimiana na kupiga gumzo huku wakiteremsha kikombe cha kahawa.
Hata hivyo, kidudu-mtu alimuona na moja kwa moja akamrushia mkewe umbea, naye akachukua simu na kumtumia mumewe ujumbe mkali akimlaumu kwa kurudiana na ex wake.
Jamaa alipopata ujumbe huo alimuaga demu na kuelekea moja kwa moja nyumbani ambako alimpata mkewe akiwa amenuna kama kaimati moto.
Mwanadada alimfokea vikali kabla ya jamaa kumweleza alipotoshwa na aliyempa umbea.