• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Kidudu-mtu asambaza umbea kwa mke wa polo aliyekutana na ‘ex’ kisiri

Kidudu-mtu asambaza umbea kwa mke wa polo aliyekutana na ‘ex’ kisiri

NA JANET KAVUNGA

MALINDI MJINI

JOMBI wa hapa alijuta kukutana na mpenzi wake wa zamani, mkewe alipopata habari na kumfokea vikali.

Jamaa alisema alikutana na ex wake katika mkahawa, wakasalimiana na kupiga gumzo huku wakiteremsha kikombe cha kahawa.

Hata hivyo, kidudu-mtu alimuona na moja kwa moja akamrushia mkewe umbea, naye akachukua simu na kumtumia mumewe ujumbe mkali akimlaumu kwa kurudiana na ex wake.

Jamaa alipopata ujumbe huo alimuaga demu na kuelekea moja kwa moja nyumbani ambako alimpata mkewe akiwa amenuna kama kaimati moto.

Mwanadada alimfokea vikali kabla ya jamaa kumweleza alipotoshwa na aliyempa umbea.

  • Tags

You can share this post!

Hatubahatishi, tutaandaa AFCON ya kupigiwa mfano asema Ababu

Wakazi wa Rabai wapigwa kimaisha minazi ikikauka

T L