Na MWANDISHI WETU
WITU MJINI
UJANJA wa machali wa hapa kutumia ugonjwa wa demu kumtongoza uligonga mwamba mwanadada alipowafokea na kuwataka wakome kumtembelea.
Binti wa watu aliwatimua mabarobaro hao waliofika kumtakia nafuu kila mmoja alipoanza kumweleza anavyompenda.
Inasemekana demu aliugua siku chache na akawa haonekani mtaani.
Ingawa kila mmoja alidai alitaka kujua hali ya kiafya ya mwanadada huyo, aligundua walikuwa wakitaka kumwonyesha jinsi wanavyomjali ili kumwingiza boksi.
“Sitaki kuwaona hapa kwangu. Mnajifanya kunijulia hali lakini mwataka kunitongoza na kuchomeana picha!” demu aliwaka mapolo wawili walipokutana kwake.
Subscribe our newsletter to stay updated